Ijumaa, 30 Juni 2017

organized-closet
Mara nyingi unaweza kukuta mtu ana kabati limejaa nguo hadi zinakosekana pa kuwekwea na katika hali halisi anajiona hana nguo za kuvaa. Hali  hii inatokana na kukosa mpangilio wa nguo kwenye kabati na pia kuweka nguo ambazo hazihitajiki tena. Nguo zisipokuwa na mpangilio maalumu ni ngumu sana kutafuta nguo gani uivae na ipi maana hujui ipo upande gani wa kabati. Pia pale unapohifadhi nguo ambazo unajua hutazivaa tena inasababisha kabati kujaa bila sababu. Njia hizi zitakusaidia katika kupanga kabati lako:
1. Tafuta siku ambayo unamuda wa kutosha na toa nguo zako zote kabatini kisha tenga zile ambazo unahitaji kuzivaa na zile ambazo unaona hutazivaa tena ( iwe zimekubana, zimechakaa, hauzitaki tena n.k).
2. Tafuta mfuko safi uweke nguo zote ambazo hutazivaa tena ambazo upo tayari kugawa kwa wenye uhitaji. Ni vyema ukianzia nyumbani mwako, kama una dada wa kazi unaweza mpa zile ambazo zitamfaa na kisha nyingine ukapelekea wengine wenye mahitaji unaowafahamu kama ni kanisani au mahali popote pale. Ila jihadhari usimpe mtu nguo iliyochakaa sana, haipendezi.
3. Nguo ambazo unazihitaji zitenge katika makundi (blauzi, sketi, magauni, n.k) na kisha uzikunje vizuri na kuzipanga kabatini kila kundi sehemu yake. Hii itakusaidia ukiwa unatafuta gauni unajua uangalie sehemu gani.  Nguo zinazoendana pamoja kama suti au vitenge ni vyema zikawekwa pamoja sketi na blauzi yake. Kama kabati lina nafasi kubwa makoti ya suti yakiwekwa kwenye henga yanapendeza zaidi.
4. Vitu kama mikanda, skafu, mitandio n.k viwekwe mahali pake ili iwe rahisi kupatikana pale vinapohitajika.

Jitahidi uwe na tabia ya kupanga nguo zako kila unapozifua. Ilikuepuka kutafuta nguo asubuhi na hatimaye kuharibu mpangilio wa kabati lako ni vyema kama utakuwa na utaratibu wa kunyoosha nguo za wiki zima kila mwisho wa wiki, hii itaokoa muda na ‘stress’ za kutafuta nguo ya kuvaa kila asubuhi.

by AGUSTINO HAMIS 

Wanachama Wa chama cha waandishi Wa habari Manyara wakiwa katika mkutano mkuu Wa chama hicho katika ukumbi Wa community center Mbulu mjini


Jumanne, 23 Mei 2017


HABARI

Nape: Niliunda kamati kuchunguza tukio la uvamimizi, sio RC


Aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amesema kamati aliyounda ilikuwa kwa ajili ya kuchunguza tukio la uvamimizi wa Clouds Media na sio RC wa Dar es Salaam.

Nape Nnauye
Ukupitia mtandao wa twiter Nape ameandika, ‘Niliunda Kamati Kuchunguza tukio la kumamiwa kituo cha utangazaji sio kumchunguza RC. Kama RC alikuwa mmoja wa wavamizi, hayupo juu ya sheria!.

Hiyo jana Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda akiwa Star Tv kwenye kipindi cha Tuongee Asubuhi alikana tuhuma zinazomkabali kuhusu uvamizi na kuongeza kuwa kamati iliyoundwa haikuwa na mamlaka ya kumuhoji.
“Sijawahi kuvamia kituo chochote kile cha runinga , nafasi yangu kama mkuu wa mkoa naweza kumuita mtu yoyote, nina maswali kama 50 kwenye lile neno ‘Kuvamia’ la kwanza wanasema nilivamia kipindi kirushwe wakati kipindi kile kilikuwa kiko live, Watanzania kama hapa tuko live hivi mtu unaweza kuvamia kweli wakati tuko live.” alieleza.

HABARI

Rais wa Korea Kusini afikishwa mahakamani kuanza kesi




Baada ya kukamatwa mwezi machi mwaka huu na kushitakiwa makosa mbali mabali ikiwemo la rushwa mwezi April mwaka huu, hatimaye Park Geun-Hye amefikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza mjini Seoul kwa tuhuma za ufisadi.

Park Geun-Hye alifikishwa mahakamani
Park mwenye miaka 65, ameonekana hadharani kwa mara ya kwanza akiwa mahakamani hapo na rafiki wake wa karibu Choi Soon-Sil, tangu aondolewe madarakani.Park anatuhumiwa kwa kujipatia fedha kutoka kwa makampuni makubwa makubwa nchini humo.
Park Geun-Hye aliwa amekaa upande wa kushoto na amevalia ngua ya dark blue huku Choi Soon-Sin akiwa amekaa kulia na amevalia ngua kama nyeupe.
Park alipokuwa mahakanai aliulizwa swali kuwa akjira yake ni nini na nakajibu han na ahajaariwiwa,Rais Park na rafiki yake Bi Chai hawakuongea chochote na waandishi bali walikaapembemni na mawakili wao na kuzungumza na hao tu, hata wawili hao wahakuvaa sare za wafungwa kama walizovaa wakiwa garezani ila walivaa mavazi ya kawaiada.
Park ndiye rais wa tatu wa zamani Korea Kusini kukamatwa kwa tuhuma za kuhusika katika uhalifu, shirika la habari la Yonhap limeripoti.

Twiga yaendelea na mazoezi



Wachezaji wa Twiga Stars wanaendelea na Mazoezi kwenye uwanja wa Karume, wakiwa chini ya kocha Mkuu Sebastian Nkomwa.

BY HAMZA FUMO

BURUDANI


Sijawahi kuwa teja wa dawa za kulevya – Young Dee





Baada ya uliokuwa uongozi wa zamani wa Young Dee ‘MDB’ kudai waliachana na rapa huyo kwa madai ya kurudia kutumia dawa za kulevya, Yound Dee amedai hajawahi rudia kutumia dawa za kulevya huku akidai yeye hakuwahi kuwa muathirika wa dawa za kelevya. Pia rapa huyo amefunguka kuhusu familia yake, uongozi wake mpya pamoja na wazani.

BURUDANI


Hii ndio ngoma iliyomtangaza zaidi Joh Makini kimataifa


Mkali wa muziki wa Hip Hop kutoka kundi la Weusi, Joh Makini amesema kolabo yake na AKA ‘Don’t Bother’ imemtangaza zaidi kimataifa na kumpa heshima.

Joh Makini na AKA
Joh makini amesema kolabo hiyo imemuongezea thamani na imemtambulisha nje kwa kiwango kikubwa sana, mpaka anapata air time kwenye nchi kama South Africa na watu wanamjua kwa kiwango fulani, ni kwa sababu ya kolabo hiyo.
“Ukitaja wasanii ambao wapo mainstream pale South Africa huwezi kuacha kumtaja AKA, kiasi kwamba hata wasanii wa pale kumpata kwa kolabo inakuwa ni ngumu,” Joh Makini ameimbia Clouds Fm na kuongeza.
“Kufanya kazi na mtu kama yule kwanza inakutengenezea Respect alafu inaonyesha userious ulionao na watu lazima waheshimu hilo, unapofanya kazi wasikuchukulie poa. Hatujawahi kuongea kwamba tutoe ngoma yake au yangu pengine siku za mbeleni,” amesema Joh Makini.