Jumanne, 23 Mei 2017

Kunani Kagera Sugar?

Kunani Kagera Sugar?


Lazima klabu kama Kagera Sugar na Tanzania Prisons na hata JKT Ruvu zijiulize sana kwanini timu zingine zinapata udhamini halafu wao wapo wapo tu.
Stand United wamekuja kwenye ligi wakapata deal ya bin slum na baadae ya acacia.
Mbeya city wamekuja wamepata deal ya bin slum wana ya coca cola na sasa wana hii sportsmaster cjui
Singida kaja amepata patnership na NMB na leo Sportpesa
Timu zote hizi zimezikuta Kagera Sugar, Tanzania Prisons na JKT Ruvu ambazo kwa pamoja na simba na yanga zimedumu kwenye ligi kwa muda mrefu
Ni wakati wa hizi timu kujitathmini na kukaribisha mawazo mapya ya kuzisogeza mbele kagera wana wachezaji wazuri wana kocha mzuri wamemaliza msimu nafasi ya tatu wakipata changamoto mpya wanaweza hata kuwania ubingwa namaanisha kuwania sio kutwaa kwa achievement ya msimu huu wanaweza kabisa.
Mbao FC wameingia ligi kuu msimu huu na kulamba mkataba mfupi na Cowbell sambamba na Ruvu Shooting wakiwaacha wakongwe kibao . Ni dhahiri kujitathimini kunahitajika kwa kiwango kikubwa
.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni